Vinasaba Quotes

Quotes tagged as "vinasaba" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Kuna siri ambayo wanaume hawaijui kuhusu wanawake. Wanawake wenye umri wa miaka kumi na nane hadi ishirini na mbili wana mapenzi ya kweli. Ishirini na mbili hadi ishirini na nne wana mawenge. Ishirini na nne hadi ishirini na saba wanajitambua. Ishirini na saba hadi thelathini wana hofu na mashaka mengi. Thelathini hadi thelathini na tano wana msongo wa mawazo. Thelathini na tano hadi arobaini na mbili ndoa nyingi huvunjika. Kwa hiyo, kuwa makini na wanawake na wanaume hasa wanawake na wanaume wa kundi la sita. Wanawake na wanaume hasa wanawake na wanaume wa kundi la sita, wengi wao wana DNA ya wapenzi wao wa zamani.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kusudi mimba itungwe lazima kuwepo na kromosomu X na kromosomu Y. Kromosomu ni nyuzinyuzi katika kiini cha seli zenye jeni au DNA, ambazo hubeba taarifa kuhusu sifa za kimaumbile zinazorithishwa kwa kiumbe hai kutoka kwa mama na baba wa kiumbe hicho. Kwa upande wa Yesu Kristo, katika hali ya kawaida, kromosomu X ilitoka kwa Maria Magdalena na kromosomu Y ilitoka kwa malaika Gabrieli. Yesu alikuwa Myahudi lakini Kristo ni Mungu. Yesu Kristo alikuwa binadamu kama sisi, lakini alikuwa na utukufu na alikuwa na damu ya Mungu iliyotakasika. Damu kama hiyo ndiyo inayotiririka katika miili ya kila mmojawetu ijapokuwa ni damu ya Adamu, ambayo bado haijatakaswa. Damu ya Yesu si kitu kidogo. Ilipomwagika msalabani ilifunika dunia nzima. Ndiyo maana tukasamehewa. Bila damu hiyo, bila utukufu huo wa Mungu, hakuna binadamu atakayeokolewa, hakuna pepo atakayeondolewa.”
Enock Maregesi