Fataki Quotes

Quotes tagged as "fataki" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Ndani ya kibweta cha risasi kuna vitu vitano vyenye uwezo wa kulipuka kama vile risasi, kasha, baruti, kitako na fataki. Risasi hutumika kama kombora – kitu kinachoweza kusafiri hewani na kulipuka baada au kabla ya kugonga shabaha – wakati kasha kazi yake ni kuhifadhi vitu vyote vya kibweta kwa pamoja kusudi visisambae. Baruti inayotoa au isiyotoa moshi ni poda yenye uwezo wa kulipuka ambayo ndani yake kuna mkaa, salfa na shura; ambayo husukuma kombora mbele kwa nguvu kubwa baada ya fataki kulipuka kupitia katika kitako cha kibweta. Kitako cha kibweta hutumika kama kiziduo cha risasi kutoka katika chemba ya silaha, wakati fataki kazi yake ni kuwashia baruti.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ndani ya gruneti kuna vitu kumi vyenye uwezo na visivyokuwa na uwezo wa kulipuka kama vile pini, mtaimbo, springi ya mtaimbo, tundu la kuingizia baruti, baruti, fataki, fyuzi, utambi, wenzo na ganda la chuma la pingili kama vipande vya risasi. Pini inapochomolewa, na bomu kurushwa kuelekea kwenye shabaha au kuelekea sehemu nyingine yoyote, wenzo wa usalama huchomoka pia na kuachana na bomu moja kwa moja. Wenzo wa usalama unapochomoka huruhusu mtaimbo ugonge fataki ya kuwashia fyuzi kwa nguvu na kasi kubwa. Fyuzi itawaka kwa sekunde nne kabla ya kuwasha utambi, ambao utawasha baruti ndani ya sekunde moja, kabla ya baruti kulipuka – na kusambaza vipande vya bomu katika kila sehemu ya shabaha.”
Enock Maregesi